KONGOWEA


Kongowea ja mvumo, Mvita Mji wa Kale
Isokoma mititimo, na mayowe na kelele
Ni ya ngao na mafumo, na mata na panga kule
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Gongwa ni mji muovu, viovu siukalile
Hupomosha wenye nguvu, wakawa kama wawele
Ikawatia kivumvu, nyoyo zikajaa tele
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Gongwa la Mwana Mkisi*, Mvita mji wa ole
Ina waume watesi, kondo hawaiketele
Wenye ghamidha na kasi, na hasira za milele
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Kwamba mujile na kondo, kuteta na simba wale
Vumiliani vishindo, vyao msivikimbile
Simba wanayo magando, makucha wayatanule
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Ndiswi Nyali Kuu ndiswi, ndiswi msambe tufile
Ndiswi mwapigana naswi, naswi msitutawale
Ni swiswi nguli ni swiswi, tuvundao miji mile
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Kivumbi cha Kongowea, kivumapo ni ja ndwele
Walo mbali husikia, kingurumo chenda kule
Watambaji hutambia, kwa mwendo wa pole pole
Wafileo walifile, mwoleza mfu nnani?

Comments

Popular posts from this blog