PANDA Panda, panda la mnazi, lanzalo kupapatua Panda, juu ya malazi, moyo wako weshe ngowa Panda,mti wa mapenzi, uwepushie na juwa. Panda ni wako uluwa, panda darajani panda Panda, juu ya farasi, kwa haiba na sitawa Panda, kiwango mkwasi, uukimbie ukiwa Panda, situpe viasi, wendako ukikujuwa Panda ngano na mpunga, afadhali ya viliwa Panda, wimbi wa kimanga, vipawa vya wakupewa Panda usitunde changa, tauwa mbivu tauwa Panda, mwema mshajari, wite tanzu za maua Panda ,utunde johari, mwizi asijezanguwa Panda,juu ya mimbari, ulingane sawasawa. Panda, pandio zi wazi, ukenda kwea nda kwea Panda,kwamba umkwezi, weleweo ni kukwea Panda,wala pasi ngazi shimoni nakungojea Panda,futa na mtama, upate kuvundikia Panda,juu ya mkoma, vijana wakuolea Panda, dua kwa Karima, kwa utakaso na nia.
Popular posts from this blog
ITAKAPOKUKUTANA Simba ndume na wambuji, sikizani tatongoa. naketele vitongoji, na safari za mashua. Leo nakumbuka mbiji, ya kutweka na kutua. Ai,pato na mpewa, litakapo kukutana . Ai, mpewa na pato, lipalo mtu kukuwa. angawa mwana mtoto, wa kutishika kachewa. akiwa na upasito, wa kutamani ukiwa. ai, ndwele na afuwa , itakapokukutana . Ai afua na ndwele, kwa mwenye nayo kutusha. akenda mwendo wa kule, illi kutakawadhisha. aonapo yatumile, akatamani kushasha. ai ,ruhu na maisha itakapo kukutana . Ai ,maisha na ruhu, yamtumupo kiumbe. humshukuru Rabbahu, ni mpambo umpembe. kesho mbele za illahu, swiratwi isimkumbe. ai, janna na kiumbe itakapo kukutana . Ai,kiumbe na janna,mwanzo asitakiriyo. na kuuza ihisana tumwi ayaghufiriyo. apendalo akaona kwa kila atamaniyo. ai furaha na moyo itakapo kukutana . Ai, moyo na furaha alo n...
Comments
Post a Comment