AHA!

        

                  Aha!Nambe sina siha,muili wangu mzima,

                  Aha!Kutoona raha,ndipo aha!Nikasema,

                  Aha!Sambile kwa wema,nasema kwa ndwele sii,



                Aha!Si yangu mapenzi,na kwamba naona vyema,  

                Aha!Ni yao uuzi,kuua na kunguruma,

                 Aha!Nipoza mpozi,nisi kitwa wala homa.


                Aha!Vile chamba aha,hiona wangu wazazi,

                 Siwaoni kwa furaha,ila kufuta matozi,

                 Niwaza wangu jaraha,mwenyi kuwaza wazazi.         

Comments

Popular posts from this blog